Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Edward Lowassa amepongeza uteuzi
uliofanywa na Rais Dkt John Pombe Magufuli ambapo alimteua Dk. Emmanuel
Nchimbi kwa Balozi.
Akizungumza na gazeti la Jamboleo, Edward Lowassa aliyekuwa miongoni mwa
watia nia wa Chama cha Mapunduzi alisema kuwa ni jambo jema
kushirikisha viongozi kuongoza nchi huku akibainisha kuwa mbali na
uteuzi wa Dk. Nchimbi pia kuteuliwa kwa mabalozi wengine nako
kumemfurahisha.
Wakati Lowassa akisifia uteuzi wa Dk. Nchimbi, wachambuzi wengine wa
masuala ya kisiasa walisema kuwa uteuzi huo unalenga kumaliza mvutano wa
muda mrefu na mgogoro ulioibuka ndani ya CCM wakati chama hicho
kikitafuta mgombea atakaye peperusha bendera yake katika uchaguzi mkuu
mwaka jana.
Dk. Nchimbi ni mwanachama wa CCM ambaye alikuwa ni mwanamkakati katika
kambi ya Lowassa wakati wa mbio zake za kuwania kuteuliwa na chama hicho
kuwania urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.
Lowassa aliliambia gazeti la Jamboleo kuwa Dk. Nchimbi alikuwa
akionekana kama msaliti ndani ya chama hicho, lakini anaamini kufuatia
uteuzi huu shutuma hizo zitapungua. Aidha, alimsifia Dk. Nchimbi na
kusema ni kiongozi mwenye uzoefu
Siasa Yetu
Wednesday, December 7, 2016
Magufuli Kuisuka Upya CCM, Aitisha Vikao vya CC na NEC Disemba 13
Taarifa iliyotolewa Dar es Salaam jana na Kaimu Msemaji wa chama hicho, Seleman Mwenda, ilisema mkutano huo utatanguliwa na kikao cha Kamati Kuu (CC), kitakachofanyika Desemba 11 hadi 12, jijini Dar es Salaam.
Ingawa hadi sasa ajenda za vikao hivyo hazijajulikana, lakini wachambuzi wa masuala ya siasa wanasema, kufanyika kwa vikao hivyo kunatajwa kuwa ni mkakati wa Mwenyekiti wa chama hicho, Rais Dk. John Magufuli kutaka kuisuka upya CCM.
Baadhi ya wachambuzi hao wanasema uteuzi wa wajumbe watatu wa sekretarieti ya chama hicho kuwa mabalozi ni mwendelezo wa mkakati huo kuelekea uchaguzi mkuu wa ndani wa chama hicho mwakani.
Mbali na hao mjumbe mwingine wa sekretarieti, Dk Asha -Rose Migiro aliteuliwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Uingereza na nafasi yake ndani ya chama kuchukuliwa na Pindi Chana ambaye naye ameteuliwa kuwa balozi.
Katika Serikali ya awamu ya nne, Pindi Chana alikuwa Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto na baadae mwaka huu aliteuliwa kuwa Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa.
Mjumbe wa Kamati Kuu (CC), Dk. Emmanuel Nchimbi, kuteuliwa kuwa balozi kunathibitisha kuhusu uwapo wa mkakati wa Rais Magufuli kusuka upya chama hicho kwa kuweka sura mpya.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye ambaye pia ni Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi wa chama hatarajiwi kuwapo katika safu hiyo mpya, kwani tayari yupo serikalini.
Mwingine ni Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho (Bara), Rajabu Luhwavi ambaye ameteuliwa kuwa balozi anazidi kutoa taswira kuhusu mkakati wa Rais Magufuli kusuka upya chama hicho.
Katika hotuba ya Rais Dk. Magufuli baada ya kukabidhiwa uenyekiti wa chama hicho alisema miongoni mwa mambo atakayoyatekeleza ni kuimarisha utendaji kazi wa chama, huku akimnukuu hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere kwa kusema kuwa chama legelege huzaa serikali legelege.
“Nitashirikiana nanyi kujenga chama madhubuti chenye uwezo wa kuisimamia vizuri Serikali ili itekeleze ipasavyo majukumu yake, ikiwezekana tutapitia upya katiba na kanuni zetu ili kukidhi mazingira ya sasa na kuweza kuwatumikia wananchi ipasavyo.
“Tutahakikisha pia tunakuwa na safu bora ya uongozi katika ngazi zote kuanzia shina hadi taifa. Tutaangalia muundo (structure) wa chama chetu katika ngazi mbalimbali na kuondoa vyeo visivyokuwa na tija katika chama na hasa wakati huu wa mfumo wa vyama vingi” alisema Dk. Magufuli.
Dk. Magufuli alihoji kuhusu uhalali wa kuendelea kuwapo vijana wa chipukizi ndani ya chama hicho pamoja na baadhi ya safu za uongozi ndani ya chama hicho.
“WanaCCM ni lazima tujiulize je ni kweli katika zama hizi bado tunahitaji mtoto wa miaka 8 hadi 15 kuwa chipukizi kwa ajili ya kumtumia kwenye siasa badala ya kumwacha asome? Kama akiwepo chipukizi wa CCM, chipukizi wa NCCR au Chadema ama TLP tutakuwa tunajenga nchi ya namna gani?
“Je bado kuna umuhimu wa kuwa na makamanda wa vijana ambao mara nyingi wenye kupewa vyeo hivyo ni wale wenye uwezo wa kifedha pekee? Je walezi kwenye Umoja wa Wanawake (UWT) bado wanahitajika? Je washauri ndani ya Jumuiya ya Wazazi wanahitajika?" Alihoji Dk. Magufuli.
Tuesday, September 20, 2016
ZITTO Amshauri Haya Rais Magufuli Baada ya Tanesco Kushindwa Kesi ya IPTL na Kuamriwa Kulipa Sh320 Bilioni
Hukumu hiyo imetolewa na mahakama ya inayoshughulika na migogoro ya uwezekaji, ICSID yenye makao yake mjini Washington DC, Marekani na ipo chini ya benki ya dunia.
Tanesco ilikuwa ikiwakilishwa na makampuni mawili ya wawanasheria R.K. Rweyongeza & Co. Advocates na Crax Law Partners ya Tanzania, pamoja na lile la Zurich, Kellerhals Carrard.
Pesa hizo zinatakiwa kulipwa kwa Standard Chartered Bank-Hong Kong (SCB-HK).
SCB-HK ililinunua deni la IPTL kwa punguzo la bei ya milioni 76.1 kutoka Danaharta Bankin ya Malaysia, August 2005 baada ya Danaharta kushindwa kuchukua mkopo wake kutoka kwa IPTL.
Hiyo ina maana kuwa SCB-HK imepata faida ya dola milioni 172. IPTL ilikopa dola milioni 100 mwaka 1998 kutoka kwenye kundi la benki za Malaysia ili kujenga mtambo umeme Tegeta wenye megawatt 100.
TANESCO ilifungua kesi ICSID baada ya kubaini kuwa imekuwa ikitozwa zaidi na IPTL. Kesi hiyo inahusiana na ripoti ya uchunguzi wa kashfa ya IPTL iliyohusisha uchotwaji wa shilingi bilioni 306 za kitanzania.
Novemba mwaka jana, mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali wakati huo, Zitto Kabwe alisoma ripoti na kulithibitishia Bunge hilo kwamba viongozi na wafanyakazi wa serikali, wafanyabiashara, viongozi na taasisi za dini, mabenki na watu binafsi wanahusika kufanya katika ufisadifu.
Kufuatia Tanesco kushindwa kwenye kesi hiyo, Zitto amemtaka Rais John Magufuli kuchukua hatua.
“Kwanini Rais Magufuli hafanyii kazi suala la IPTL? Matapeli hawa wataendelea kuipa hasara nchi yetu mpaka lini? Sasa mahakama ya ICSID imeamua kuwa Benki ya Standard Chartered ilipwe tshs 300bn na riba. TANESCO wanaingia Hasara hii Kwa sababu ya wizi wa Fedha za TEGETA Escrow na Rais bado anavuta miguu kuchukua hatua dhidi ya suala hili. Nini kimemkuta Rais Magufuli? Rais anataka tuamini kuwa IPTL/PAP Ni kweli waligharamia Mkutano Mkuu wa CCM uliompa yeye Uenyekiti,” ameandika Facebook.
“Tanzania hapo Ni hasara tupu 1)mmelipa matapeli Fedha zilizokuwa kwenye TEGETA escrow account. 2) mmewapa mtambo wa kuzalisha umeme matapeli hao na mnaendelea kuwalipa capacity charges mpaka sasa. 3) mnawalipa standard chartered Fedha zao Kwa mtambo ambao sio wenu na Kwa Fedha ambazo mngezitoa escrow a/c lakini sasa mtazitoa hazina,” ameongeza.
“Rais achukue hatua zifuatazo – awafikishe mahakamani watu wote waliohusika na kuitia Nchi hasara katika sakata la TEGETA Escrow – aitwae mitambo ya IPTL kisheria na kuimilikisha Kwa TANESCO – amkamate Bwana Harbinder Singh Seth na wafuasi wake wote na kuwafikisha mahakamani Kwa makosa ya utapeli, wizi, uhujumu uchumi, utakatishaji wa Fedha.”
“Benki iliyotumika kupitisha Fedha za TEGETA escrow ndio ilipe Hilo deni tunalotakiwa kulipa. Rais aamue kusimama na watanzania au kusimama na matapeli wa TEGETA escrow.”
Thursday, September 15, 2016
Malawi Yadai Kuishtaki Tanzania Kwenye Umoja wa Afrika(AU)
Foreign
Affairs and International Cooperation minister Francis Katsaira said
Tanzania has released a new Lake Malawi map which shows the east African
country has taken a chunk of Lake Malawi, which is potentially rich in
oil and gas..
“We have already reported them to the African Union and very soon we will be reporting them to Comesa and Sadc,” he said.
Kasaira said Tanzanian authorities have threatened to beat up and arrest Malawians who will disregard the new map.
The old map, drawn up by Germany and Britain gives the whole Lake Malawi, except a small part to Malawi.
Tanzania has taken much interest in the lake after oil was discovered in the lake popularly known as lake of stars.
Katsaira
said both Malawi and Tanzania were supposed not to interfere with the
Lake Malawi issue as the matter was with the African Union and a
mediation team.
He
therefore said the government is waiting for a response from Tanzsnia
on the proposal for Mutharika and Magofuli to meet inorder to iron out
the misunderstanding over the lake.
Malawi disputes Tanzania’s claim to half the lake – Africa’s third biggest.
It has accused Tanzania of raising tension by allegedly intimidating Malawian fishermen on the lake.
Malawi awarded oil exploration licences to firms to search for oil in the lake, which Tanzania calls Lake Nyasa.
Gavana BOT Afichua Siri ya Kilio Cha Fedha Kupotea Mtaani
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Profesa Ndulu alisema kuwa kwakuwa taasisi hiyo ndiyo inayofahamu fedha zote zilizopo benki na zilizopo mtaani, inafahamu kuwa hakuna fedha iliyopotea bali fedha zimepotea kwa watu waliokuwa wanazipata kwa njia ya udanganyifu kwakuwa sasa Serikali imebana mianya hiyo.
“Hakuna fedha iliyopotea, Serikali imebana shughuli za watu na ‘mission town’ sasa shughuli zote zinafanywa na Serikali. Hivyo, kwao fedha zimepotea, lakini kwetu hazijapotea,” alisema Profesa Ndulu.
Hata hivyo, Profesa Ndulu alikiri kupungua kwa fedha katika mabenki nchini hali iliyopelekea kupunguza kasi ya utoaji mikopo kwa wananchi. Alisema hali hiyo ilitokana na kuhamishwa fedha za mashirika ya umma na taasisi kutoka benki za biashara kwenda BoT.
“Fedha hizo zitarudi katika benki hizo wakati zitakapopelekwa kwenye Halmashauri kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali,” Profesa Ndulu aliahidi.
Katika hatua nyingine, Gavana huyo wa Benki Kuu alisema kuwa uchumi unatarajiwa kukuwa kwa asilimia 7.2 mwaka huu, huku akibainisha kuwa moja kati ya sababu zinazopelekea ukuaji huo ni ongezeko la uzalishaji wa umeme na saraju.
Akizungumzia hali ya deni la taifa, alisema kuwa deni la taifa la ndani limeongezeka kutoka shilingi trilioni 8.6 Mwezi Desemba mwaka jana hadi shilingi trilioni 10 mwezi Juni mwaka huu.
Profesa Ndulu alibainisha kuwa wakati deni linalotokana na kukopa ndani likipaa, deni linatokana na ukopaji wa limepungua baada ya Serikali kupunguza ukopaji nje ya nchi.
Hatuhusiki Kumtafutia Mtu Ajira - Bodi ya Mikopo
Hayo yamesemwa jana Jijini Dar es salaam na Mkurugenzi Msaidizi wa Habari, Elimu na Mawasiliano kutoka Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu Cosmas Mwaisobwa wakati akijibu maswali ya wananchi kupitia kipengele cha Kikaango cha EATV.
“Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu inatoa mikopo suala la kutafuta ajira halituhusu hivyo mnufaika yoyote asiwe na kigezo kwamba hajapata kazi , hiyo siyo kazi yetu, kazi yetu ni kuwawezesha kupata elimu basi” Alisema Mwaisobwa.
Aidha Mwaisobwa alisema wanufaika wote ambao walipata mikopo wanatakiwa kukatwa asilimia 8% ya pato la mwezi, na kama mtu anafanya kazi binafsi na hakatwi popote atatakiwa kutoa kiwango cha 120,000/= na kwa ambao wamenufaika na hawataki kuanza kulipa mkopo watapigwa penati ya 10% ya mkopo kwa mwaka.
Pamoja na hayo Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu imewataka walioomba mikopo kuvuta subira kwani Bodi inasubiri majina kutoka Tume ya Vyuo Vikuu ili Bodi ya Mikopo iweze kufahamu vyuo walivyopangiwa na kiwango cha ada ili haki iweze kutendeka kwa waombaji.
Majambazi 10 yateka magari, yaua dereva
Dereva huyo, Chrispin Inyangwe (40) alipigwa risasi ya mgongoni alipojaribu kupambana nao.
Tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia jana eneo la katikati ya vijiji vya Miula na Kalundi vilivyopo Kata ya Kipande wilayani Nkasi.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, George Kyando amesema wafanyabiashara hao walikuwa wakitokea mnadani na walipofika eneo hilo walikuta mawe yamepangwa barabarani kuzuia magari.
Amesema baada ya kuona mawe hayo, magari hayo yalilazimika kusimama na ndipo majambazi hao waliokuwa na silaha za moto, mapanga na marungu walipoibuka na kufyatua risasi hewani na baadaye kutaka wafanyabiashara hao wasalimishe fedha na simu zao za mkononi.
Subscribe to:
Comments (Atom)






