Kauli hiyo imetolewa na Makamu Mwenyekiti wa chama hicho upande wa Bara
Philip Mangula wakati akizindua Daftari la Mashina ya chama hicho ambayo
ndiyo chimbuko la wanachama wake kwa lengo la kuimarisha chama hicho na
kuongeza wanachama.
Akizungumza katika uzinduzi huo uliofanyika katika kijiji cha Utiga kata
na halmashauli ya Wang'ing'ombe mkoani Njombe Mangula amesema kuwa
uchaguzi huo ulikuwa wa tofauti na miaka mingine ingawa kwa sasa
ukirudiwa utakuwa rahisi.
Katika wilaya ya Wang'ing'ombe chama hicho kinadai wa kuongoza kuwa na
wanachama wengi na kupata madiwani wote wa CCM na kuwa sasa kinazindua
kitabu hicho ili kuimarika zaidi.
Kitabu hicho kinazinduliwa pamoja na shina la chama hicho huku vitabu
hivyo vikigawiwa kwa mabarozi 125 na viongozi wa kata 24 na wanachama
lukuki wakijiunga na chama hicho na kukabidhiwa kadi za chama hicho na
Mangula.

No comments:
Post a Comment